|
Mijadala ya
kiswahili
Search Kuruani
kwa kiswahili
Radio Rahma
- Radio ya Kiislamu
Dua
Kuhusu Mambo Mbali Mbali.
Makala
Kuhusu Walio Silimu.
Simulizi
za Bibi Mahiira.
Ukumbi wa Tafsiri za Ndoto
Visa Vya
Masahaba
Mechi za leo na tv inayotoa
Mechi zichezwao sasa hivi
Mechi za kesho
kwenye tv
Mechi za
jana kwenye tv
Mechi kali
sana za wiki hii
Mechi zote
hizi kwenye Tv
Mashindano yote duniani
Matokeo ya mechi (Latest)
Kuruani Tukufu
Links
muhimu sana
Radio Rahma
Mijadala ya Kiswahili
Uislamu.org
Alhidaaya.com
Islamtz.org
Uislam.net
Ukumbi wa
Dini
Sikiliza Quran
Aqidah.Net
Dua
na Adhkaar
Makala Kuhusu Islam
Visa Vya Kweli
Yanao Wakhusu Wanawake
Maswali Majibu
Vitabu Vya Dini
Sikiliza Mawaidha
Sikiliza Kaswida
|
Hali ya Hewa Leo - Tanzania
|
Dar es Salaam
Dodoma
Kigoma
Mtwara
Mwanza
Tanga
Zanzibar
Nduli
Maruku
MItetemiaaruku
gsmhacks.com
series60v3.com
Ip-mart-forums
Mobi4all (Arabic)
Nokia Gate (Arabic)
Daily Mobile forum
| download
Program za PC Kamili |
damasgate.com (Arabic)
Alsayra Forum (Arabic)
|
| SOMA
UJIHESABU NAFSI YAKO. |
|
1.Jee, umemdhukuru Mola na
umemshukuru wakati wa kuamka kutoka
usingizini?
2.Jee, umesali leo Sala ya Alfajiri
Msikitini?
3.Jee, umesoma leo nyiradi za
Asubuhi?
4.Jee, umemuomba siku ya leo Mola
wako akuruzuku riziki ya halali?
5.Jee, umemshukuru Mola juu ya neema
ya kuwa wewe ni Mwislamu?
6.Jee, umemshukuru Mola juu ya neema
ya kuwa amekupa masikio na macho na
moyo?
7.Jee, umekifungua leo kitabu cha
Mola (Qur-ani) ukasoma baadhi ya Aya
zake?
8.Jee, umemnasihi/umenasihi kuhusu
mambo ya dini?
9.Jee, umemuomba Mola akuingize
Peponi?
10.Jee, umejikinga kwa Mwenyezi
Mungu akuepushe na Moto?
11.Jee, leo umesali Sala zako zote
Msikitini?
12.Jee, leo umemsalia Mtume S.A.W.?
13.Jee, leo umeamrisha mema na
kukataza mabaya?
14.Jee, leo ulikuwa na khushuu
katika Sala zako unajua unayoyasema?
15.Jee, umependa kwa ajili ya Mola
na kuchukia kwa ajili ya Mola?
16.Jee, leo umemuomba Mola msamaha
akusamehe madhambi yako?
17.Jee, umemuomba Mola athibiti moyo
wako juu ya dini Yake?
18.Jee, leo umemtabasamia katika uso
wa ndugu yako Mwislamu.
19.Jee, umeusafisha ulimi wako
kutokana na uongo, na kusema watu na
kusema maneno ya upuuzi?
20.Jee, umeusafisha moyo wako
kutokana na maradhi ya hasad n.k.
21.Jee, umeuzoesha moyo wako tabia
njema kutokana na subira, uchaMungu,
huruma kumtegemea Mola na ikhlaasi?
22.Jee, umekumbuka mauti na kaburi
na siku ya Kiyama?
By
Rashid Al-Shuely
|
|
Abdun-Naaswir
Hikmany
Tofauti yetu na wasio kuwa Waislam si chengine kipya ila ni tabia. Uzuri
wa mwenendo wa maisha yetu ndio utakaotupatia sifa mbele ya jamii
isiyokuwa ya Waislam. Hima yetu ya kutosema uongo na kufuata maadili ya
ajabu ndio utakuwa msingi imara wa imani yetu. Haya yote yameelezwa na
Habiybul Mustwafaa (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa
hakuletwa yeye isipokuwa kurekebisha jamii kuwa na tabia njema.
Hakika Uislamu wetu umekamilika kwa kuwa na tabia bora za kuigwa na
Waislam wenyewe kwa ushahidi wa Qur-aan na Sunnah.
Kama kweli sisi ni Waislam tunaoipenda diyn yetu ni lazima tuwe tayari
kuanza kubadilika kila hatua ya maisha yetu kwa kuishi Kiislam. Zingatio
letu litatupeleka hatua baada ya hatua ili kurekebisha nyumba
iliyojikita kwenye masuala yasioendana kabisa na mila zetu sisi Waislam.
1. TUZUNGUMZE KIISLAM
Muislam wa kweli ni lazima awe ni mkweli, hatakiwi kuzua uongo,
kufitinisha, kusengenya wala kuzungumza kwa sauti ya juu.Haya tunayapata
ndani ya Qur-aan:
{{Na uteremshe sauti yako; bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko
sauti zote (kwa makelele yake ya bure).}} [Surat Luqmaan: 19]
Pia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuhimiza sana
kushikamana katika kusema ukweli:
“Shikamaneni na ukweli, kwani ukweli unapeleka katika wema, na wema
unapeleka Peponi.” [Muslim]
2. TULE KIISLAM
Muislam anatakiwa ale kilicho mbele yake kwa kutumia mkono wa kulia na
asiwe na papara ya kusukuma tonge namna ya kima anavyokula. Aanze kula
kwa kusema “BismiLlaah” na amalize kwa kusema “AlhamduliLlaah”. Chakula
cha Muislam ni lazima kiwe ni cha halali, hatakiwi kula ovyo ovyo kama
wanavyofanya wasiokuwa Waislam. Anapokula aligawe tumbo lake kwenye
thuluthi tatu. Thuluthi moja ni ya chakula, nyengine ni ya maji na
mwisho ni hewa. Hii ni kwa mujibu wa dalili ya Hadityh:
"Kama ukilazimika kula hakikisha theluthi moja ya tumbo lako unaijaza
chakula, theluthi moja maji na acha theluthi moja kwa ajili ya hewa (yaani
iache tupu)” (At-Tirmidhiy).
3. TUSIKILIZE KIISLAM
Muziki ni haramu na haifai kwa Muislam kuutengeneza, kutengenezewa,
kuimba, kuimbiwa, kuutangaza, kuupeleka muziki, kuuza, kula thamani yake,
kununua na kuuza. Muziki umekuwa ni tatizo kubwa kwa Waislam kwani
wengine hata usingizi hawapati bila ya kusikiliza muziki. Nyumba za
Kiislam sasa zimekuwa sawa na magofu kwa kutopatikana maadili ya Kiislam.
Kwani wengi wanaishi tofauti na mafundisho ya Mtume (Swalla Allaahu
‘alayhi wa aalihi wa sallam). Ni muhimu kwa Waislam wakawa wanasoma
Qur-aan kila siku kwa sauti na kwa kusikilizana kwa mtindo wa dawaar (mmoja
baada ya mwengine). Tuzibadilishe nyumba zetu kwa kusikiliza idhaa za
Kiislam zisizokuwa na mambo ya uchafu na uzushi.
((Na soma Qur-aan kwa utaratibu na utungo)) [Al-Muzammil 73: 4]
Muislam anayesoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika na Mitume (‘Alayhi
swalaatu was-salaam). Hata yule asiyejua kusoma Qur-aan ni vyema akawa
na jitihada ya kujifundisha ilhali anakosea au hata kuchekwa. Amesema
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((Yule ambaye kwamba anasoma Qur-aan naye ni mjuzi (hana shida aina
yoyote) atakuwa pamoja na Malaika na Mitume (‘Alayhi swalaatu
was-salaam) na watiifu. Na yule ambaye kwamba anarudia pamoja na kuwa na
shida katika kusoma basi atakuwa na ujira mara mbili(( [al-Bukhaariy,
Muslim, Tirmidhy na Ibn Maajah kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah (Radhiya
Allaahu 'anha)]
4. TUVAE NA TUTEMBEE KIISLAM
Maringo ya kutembea bila ya shaka yanatokana na mtu kuvaa nguo za
kifakhari ambazo hazitakiwi kuvaliwa kwa Muislam. Muislam wa kiume
anatakiwa avae nguo zisizoburura. Mwanamke hatakiwi kuonekana zaidi ya
viganja vya mikono na kipaji cha sura yake. Mapambo yote ni halali kwa
mumewe na walio Maharimu wake. Haitakikani Muislam kutembea kwa kujivuna,
kujifakharisha na maringo. Hivi sivyo Uislam unavyotufundisha kuishi.
Qur-aan inasema:
{{Wala usitembee katika ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua
ardhi wala huwezi kufikia urefu wa milima}} [Surat Israa: 37]
Usiwaangalie watu kwa jeuri au kwa upande mmoja wa uso. Allaah (Subhaanahu
wa Ta’ala) Anasema:
{{Wala usiwatazame (usiwafanyie watu jeuri), kwa upande mmoja wa uso,
wala usende katika ardhi kwa maringo, hakika Mwenyezi Mungu hampendi
kila ajivunaye, ajifaharishaye.}} [Surat Luqmaan: 18]
5. TUJENGE URAFIKI WA KIISLAM
Miongoni mwa matatizo makubwa ya vijana wetu pamoja na Waislam kukosa
maadili ya Kiislam ni kuwa na marafiki wasiokuwa na maadili mema. Ni
vyema Muislam akawa hana rafiki hata mmoja kuliko kuwa na marafiki kumi
wasioishi Kiislam. Kuishi Kiislam yatakikana juhudi na inaanza kwa kuwa
na rafiki mwema atakayekukemea unapofanya kosa na kukupa maneno ya subra
wakati wa huzuni.
Lazima tuchague marafiki ambao wako radhi na dini yetu na tuepukane na
wale ambao hawako radhi na dini yetu. Na tukiona marafiki zetu matendo
yao sio mazuri, ni lazima tuepukane nao kwa sababu tunaweza tukaiga
tabia zao ambazo zinakwenda kinyume na dini yetu.
Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu
yamkini kufuata dini ya rafiki yake, kwa hivyo muangalie unayemfanya
rafiki.” (Abuu Daawuud na Tirmidhiy)
6. TULALE KIISLAM
Tumalizie kwa kuona namna anavyotakiwa Muislam kuimaliza siku yake kwa
kujipumzisha Kiislam. Muislam anatakiwa atie wudhuu kabla ya kulala,
wudhuu unaendana na Sunnah ya kupiga mswaki. Ni vizuri ukaswali rakaa
tatu za witri (kwa wasioamka usiku).
Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akienda
kulala usiku anakusanya viganja vyake kisha akivipuliza na akivisomea
Suratul-Ikhlaas, na Suratul-Falaq, na Suratu-Nnaas, kisha akipangusa kwa
hivyo viganja vyake kiasi anachoweza katika mwili wake, akianza kichwani
na usoni na mbele (akifanya hivyo mara tatu).
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Ukienda
kulala soma Ayatul-Kursiy mpaka uimalize kwani Mwenyezi Mungu
Ataendeleakukuhifadhi wala hakukaribii shetani mpaka asubuhi”
Unapolala ulaze ubavu kwa upande wa kulia na usome du’aa ifuatayo:
اللّهُـمَّ أَسْـلَمْتُ نَفْـسي إِلَـيْكَ، وَفَوَّضْـتُ أَمْـري إِلَـيْكَ،
وَوَجَّـهْتُ وا جْـهي إِلَـيْكَ، وَأَلْـجَـاْتُ ظَهـري إِلَـيْكَ،
رَغْبَـةً وَرَهْـبَةً إِلَـيْكَ، لا مَلْجَـأَ وَلا مَنْـجـا مِنْـكَ إِلاّ
إِلَـيْكَ، آمَنْـتُ بِكِتـابِكَ الّـذي أَنْزَلْـتَ وَبِنَبِـيِّـكَ
الّـذي أَرْسَلْـت
“Ewe Mwenyezi Mungu nimeisalimisha nafsi yangu kwako, na nimekuachia
mambo yangu Wewe na nimeuelekeza uso wangu kwako na nimeutegemeza mgongo
wangu kwako, kwa matarajio na kwa kukuogopa, hapana sehemu ya kukimbilia
wala ya kujiokoa ila kwako, nimekiamini kitabu chako ulichokiteremsha na
Mtume wako uliyemtuma”.
Na hizi hapa ni Nyiradi za kulala.
Bila ya shaka tutakapoishi Kiislam tutakuwa mbali na wasiokuwa Waislam.
Hivyo maisha yetu yatakuwa hakika ni ya Kiislam. Kila kitu yatakikana
juhudi na inaanza kwa nafsi kujifunga kukubali mafundisho ya Kiislam.
Inawezekana kubadilika kwa kuishi Kiislam. Anza sasa, katu usichelewe
kuishi Kiislam.
|
Gazeti la Mwananchi
Gazeti la Uhuru
Gazeti la
An-nuur
Gazeti la Raia Mwema
Arusha Times
Gazeti la Majira
Gazeti la Maisha
Gazeti la Dimba (Sports)
Gazeti la
Bingwa
Gazeti la
Mwanaspoti
Gazeti la Mtanzania
The Citizen Newspaper
Moja Newspaper
The Express - Tanzania
Daily Nation
Globalpublishertz
The
African Paper
The
East African
Newspapers in IPPMedia
Sekenke Forums
Swahili News
TZ Website
Addresses
Habari Tanzania
Dictionary ya Kiswahili
Ipp Media
BBC Swahili Site
Wazanzibari Maarufu
Oman Observer
Oman NewsPaper
Times Of Oman
Alshabiba
Almalaib
Al-Watan
Oman Tribune
Nizwa Magazine
Oman News Agencyimes
Business Today
The Week
| Frequencies
za Satelitte. |
ArabSat
(Badr C/3/4)
Nilesat 101/102
Channel
Mpya (Headlines)
Satelitte
Mpya (launches)
| Satelitte
Sites, DVB, Receivers. |
ProgDVB
Site
dvbskystar.com
dvbsoft.net
Digital PC Receiver Cards
skystar.org
dvbsupport.net
dvbsoft.eu
fannansat
(Arabic)
kingofsat.net
Links
Adam
Al Rustaq
As Sib
Bahla
Buraimi
Fahud
Haima
Ibra
Khassab
Marmul
Masirah
Matrah
Muscat
Nizwa
Qairoon Hairiti
Saiq
Salalah
Samail
Sohar Majis
Sur
Thumrait
Taqah
Omantel Website
Oman Visa Form
Read Omantel Email
Omanmobile
Website
Nawras WebSite
Arabian Oryx Project
Census 2003
Dhofar Municipality
Muscat Municipality
Ministry of Commerce
Ministry of Education
Ministry of Health
Ministry of Awqaf
Ministry of Transportation
Ministry of Housing
Ministry of Justice
High Education
Ministry of Oil & Gas
MCT Securities Market
Muscat Inter Book Fair
Oman IT Task Force
Oman Radio
Oman Television
Oman Air
Sultan Qaboos University
|